Kulalama
Dunia huwa inatupa kile tunachokitaka na tunakizungumzia kila mara katika midomo yetu. katika jamii zetu kulalamika ndiyo utamaduni uliozoeleka, ukienda ofisini watu wanalalamika, kwenye usafiri watu wanalalamika, kwenye nyumba za ibada watu wanalalamika. Hivi ni eneo gani la maisha yako umeona sehemu ambayo watu hawana utamaduni wa kulalamika? Binadamu tumekuwa ni watu ambao tumekosa shukrani, hata tupewe nini hatuwezi kukosa shukrani. Tunajiona hatuna kitu fulani kwa sababu maisha yetu tumeyaweka katika vitu, tunaishi kwa ulinganishi wa vitu na pale tunapojaribu kulinganisha tunajikuta tunaumia na hatuna kitu. Hakuna mtu ambaye amejitosheleza kwa kila kitu, tunatakiwa kushukuru kwa kile ambacho kipo ndani mwetu, tusiangalie tumekosa nini, badala yake tukumbuke tumepata nini, tukiwa tunaangalia vile ambavyo tunavyo maisha ni mazuri sana lakini tukiwa tunaangalia vile ambavyo hatuna maisha yanakuwa siyo mazuri sana. Tunapoteza maana ya maisha yetu pale tunapokuwa tunajilinganisha...